We answer listener questions about the making of Season 5: Hark and of Threshold more broadly in this special AMA episode with host Amy Martin, managing editor Erika Janik, and producer Sam Moore. Thanks to Kraftkabel for the use of his music. You can find the whole track here . Threshold is nonprofit, listener-supported, and independently produced. You can support Threshold by donating today . To stay connected, sign up for our newsletter .…
เนื้อหาจัดทำโดย Iran.Tanzania เนื้อหาพอดแคสต์ทั้งหมด รวมถึงตอน กราฟิก และคำอธิบายพอดแคสต์ได้รับการอัปโหลดและจัดหาให้โดยตรงจาก Iran.Tanzania หรือพันธมิตรแพลตฟอร์มพอดแคสต์ของพวกเขา หากคุณเชื่อว่ามีบุคคลอื่นใช้งานที่มีลิขสิทธิ์ของคุณโดยไม่ได้รับอนุญาต คุณสามารถปฏิบัติตามขั้นตอนที่แสดงไว้ที่นี่ https://th.player.fm/legal
Player FM - แอป Podcast
ออฟไลน์ด้วยแอป Player FM !
ออฟไลน์ด้วยแอป Player FM !
พอดคาสต์ที่ควรค่าแก่การฟัง
สปอนเซอร์
Iran-Tanzania Podcast
ทำเครื่องหมายทั้งหมดว่า (ยังไม่ได้)เล่น…
Manage series 3382153
เนื้อหาจัดทำโดย Iran.Tanzania เนื้อหาพอดแคสต์ทั้งหมด รวมถึงตอน กราฟิก และคำอธิบายพอดแคสต์ได้รับการอัปโหลดและจัดหาให้โดยตรงจาก Iran.Tanzania หรือพันธมิตรแพลตฟอร์มพอดแคสต์ของพวกเขา หากคุณเชื่อว่ามีบุคคลอื่นใช้งานที่มีลิขสิทธิ์ของคุณโดยไม่ได้รับอนุญาต คุณสามารถปฏิบัติตามขั้นตอนที่แสดงไว้ที่นี่ https://th.player.fm/legal
Audio za Kituo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
…
continue reading
12 ตอน
ทำเครื่องหมายทั้งหมดว่า (ยังไม่ได้)เล่น…
Manage series 3382153
เนื้อหาจัดทำโดย Iran.Tanzania เนื้อหาพอดแคสต์ทั้งหมด รวมถึงตอน กราฟิก และคำอธิบายพอดแคสต์ได้รับการอัปโหลดและจัดหาให้โดยตรงจาก Iran.Tanzania หรือพันธมิตรแพลตฟอร์มพอดแคสต์ของพวกเขา หากคุณเชื่อว่ามีบุคคลอื่นใช้งานที่มีลิขสิทธิ์ของคุณโดยไม่ได้รับอนุญาต คุณสามารถปฏิบัติตามขั้นตอนที่แสดงไว้ที่นี่ https://th.player.fm/legal
Audio za Kituo cha Utamaduni cha Jamhuri ya Kiislamu ya Iran
…
continue reading
12 ตอน
ทุกตอน
×Musharraf al-Din Mosleh ibn Abdullah ibn Musharraf, ambaye baadaye alijulikana kama Saadi Shirazi, ni mmoja kati ya malenga na mshairi mkubwa na mashuhuri nchini Iran. Wanahistoria wanaamini kwamba Saadi Shirazi alizaliwa kati ya mwaka 600 na 610 Hijiria (sawa na takriban mwaka 1210 Miladia). Walakini, hakuna tarehe kamili inayojulikana ya kuzaliwa kwa malenga huyu, ingawa wanahistoria wanakadiria mwaka huo wa kuzaliwa kulingana na athari za kazi zake. Saadi alizaliwa katika familia ya wanazuoni, wasomi na watu wenye maadili mema. Baba yake alikuwa mfanyakazi wa Mahakama ya Atabak na Shah Saad bin Zangi. Wengine wanaamini kwamba mshairi huyu amechagua jina la ukoo la Saadi kama ni mtu mwenye utambuzi wa haki. Mbali na kuhudumu katika mahakama, baba yake pia alikuwa akijishughulisha na masuala ya kidini na alikuwa akimshajiisha mno mtoto wake kujifundisha elimu ya kisekula na kidini pia. Kwa msaada wa baba yake, Saadi alipata ujuzi wa kina katika nyanja za historia na fasihi. Wakati wa kuzaliwa kwake, mtawala wa Shiraz alikuwa mfalme wa tatu wa serikali ya Atabakan. Nguvu ya Waseljuk ilipodhoofika siku baada ya siku katika kutawala nchi, uliibuka mlolongo wa utawala wa kieneo. Mbali na Shiraz, Atabak pia alikuwa na nguvu za kiutawala huko Damascus, Mosul, Aleppo (Halab), Mesopotamia ( Furati na Hidekeli), na Azerbaijan. Baba yake Saadi alifariki dunia, wakati Saadi akiwa na umri wa miaka 12, na babu yake mzaa mama, Massoud ibn Mosleh, alichukua jukumu la kumlea na kumtunza mjukuu wake. Katika wasifu wa Saadi, tunasoma kwamba baada ya mshairi huyu kujifunza misingi ya elimu ya kidini na fasihi huko Shiraz, alikwenda Baghdad akiwa bado barobaro na kijana chini ya usimamizi wa Atabak na akajiunga katika madrasa ya Nidhamiyyah. Shule hii ilikuwa inatoa elimu maalumu kwa watu wanaotaka kujikita zaidi katika nyanja za fiqh ( sheria za Kiislamu) na falsafa. Wanazuoni wakubwa kama vile Suhrawardi walimlea kielimu Saadi katika madrasa hiyo. Baada ya kumaliza mafunzo, Saadi akaazimia kufanya safari katika maeneo ya Hijaz, Sham na Syria kwa lengo la kupata elimu na uzoefu zaidi. Baada ya hapo akashika njia na kuelekea Makka. Wakati huo huo, alifanikiwa kufunga ndoa, na kisha alifanikiwa kupata mtoto, lakini baada ya kumpoteza mtoto wake huyo, Saadi aliamua kusafiri tena ili kuvumilia mateso hayo, mateso ambayo yalimfanya awe mwenye kupenda zaidi mashairi. Saadi alitembelea miji mbalimbali duniani kote na huko alijishughulisha zaidi na kufundisha na kuhubiri katika miji hiyo. Wataalamu wengine wa historia wamethibitisha kufanya safari yake ya India na sehemu nyingine kadhaa za dunia, na wanaeleza kuwa, safari hizo zilidumu takriban miaka 30. Hata hivyo, muda wa safari na maeneo aliyotembelea Saadi, ni mambo ambayo bado yanatiliwa shaka mno. Hatimaye, baada ya kupita miaka mingi na kupata uzoefu wa kutosha, malenga huyu aliamua kurudi katika nchi yake na mji wake wa asili wa Shiraz. Wakati wa kurejea kwake Shiraz, Abu Bakr ibn Sa'd, mfalme wa Atabaki, alikuwa akitawala huko Shiraz wakati huo. Na kulingana na baadhi ya maelezo ya watu, mshairi huyo alichukua jina la ukoo wa Saadi kutoka kwa jina la mfalme (Saad). Baada ya Saadi kurejea Shiraz, mshairi huyu alianza kuandika na kukusanya kazi zake. Kazi yake ya kwanza aliyoiandika ilikuwa kuandika kitabu cha mashairi alichokipa jina la Bustan, mnamo mwaka 655 Hijria, na kukabidhi mkusanyiko wa mashairi hayo kwa mfalme aliyekuwa akitawala kipindi hicho aitwaye Abubakar ibn Sa'd Zangi. Kitabu cha mashairi cha Golestan kilichoandikwa na malenga huyu mkubwa kilitungwa mwaka wa 656 Hijiria, mwaka mmoja baada ya kuandikwa kwa kitabu cha Bustan. Saadi alikamilisha uandishi wa mashairi ya kitabu hicho kwa muda mfupi. Kuandikwa kwa vitabu viwili katika muda mfupi kunaonyesha kwamba, kwa kiasi kikubwa mashairi hayo yalikuwa yameshatayarishwa mapema, bali alichokifanya ni kukusanya na kufanya masahihisho katika hatua za mwisho kabla ya kuchapishwa. Mengi yamesemwa kuhusu Saadi juu --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message…
ATTAR NEYSHABURI MALENGA WA KIIRANI Tarehe 25 Farvardin kwa mujibu wa ( Kalenda ya Kiirani) inayosadifiana na tarehe 14 Aprili, ni siku ya kumkumbuka na kumuadhimisha malenga wa Kiirani Farid al-Din Abu Hamid Muhammad bin Abu Bakr Ibrahim bin Is- haq Attar Neyshabouri, ambaye ni mmoja wa washairi mashuhuri, aaref na mwanafikra mkubwa wa Kiirani aliyeishi mwishoni mwa karne ya sita na mwanzoni mwa karne ya saba Hijria. Baadhi ya wanahistoria wameandika kuwa, mwanafikra na malenga huyo wa Kiajemi amezaliwa mwaka 513 na wengine wanaeleza kuwa alizaliwa mwaka 537 Hijiria. Attar Neyshabouri alizaliwa katika kijiji cha Kadkan au Shadiakh, ambacho wakati huo kilikuwa sehemu ya jiji la Neyshabour. Hakuna habari inayoelezea taarifa zake za utotoni mwake, isipokuwa baba yake aliishi katika mji wa Shadiakh akifanya kazi ya kuuza dawa za asili, na alikuwa mahiri na hodari mno katika biashara hii ya kuuza dawa za asili, na baada ya kufariki dunia baba yake, Farid al Din Attar Neyshabouri aliendeleza shughuli za marehemu baba yake ya kuuza dawa za asili. Wakati akishughulika na uuzaji wa dawa za asili Attar Neyshabouri alikuwa akitoa tiba ya asili na wala haijulikani utaalamu huo wa kutoa tiba ya asilii aliupata kutoka kwa nani. Attar Neyshabouri aliendelea na shughuli zake za kutoa tiba ya asili sanjari na kuuza dawa za asili hadi pale yalipopatikana mapinduzi ya kiroho na kimaanawi kwa upande wake, na jambo hili limebainishwa kwa kutolewa visa kadhaa, lakini kisa maarufu ni hiki kifuatacho: “Siku moja Attar Neyshabouri alikuwa dukani kwake akifanya shughuli zake, mara akaingia “Darwesh" na akaanza kusema maneno kadhaa yanayohusiana na Mwenyezi Mungu, ili Attar aweze kuvutika na kumsaidia, lakini Darwesh hakupata msaada wowote kutoka kwa Attar Neyshabouri. Darwesh akamwambia Attar : Ewe kijana unataka ufariki duniani kwa kifo cha namna gani? Attar akajibu: Kwa njia ileile ambayo wewe unataka kufa. Darwesh akasema; Wewe unataka kufa kama nitakavyokufa mimi? Attar akajibu: Ndio, Darwesh akachukua bakuli lake lililotengenezwa kwa mbao na kuliweka chini ya kichwa chake na akasema maneno ya Mwenyezi Mungu na hatimaye kufariki dunia. Kwa vile Attar Neyshabouri aliliona tukio hilo kwa macho yake aliathirika mno na kubadilika na akaamua kutoka dukani na kubadilisha kikamilifu mtindo na mwenendo wa maisha yake” . Attar Neyshabouri aliposhuhudia tukio hilo la Darwesh , akaacha kabisa shughuli za tiba na biashara za dawa za asili, na akaamua kuelekea kwa Sheikh Mkuu Aref Rukniddin Akaf , wakati huo Sheikh Aref alikuwa mtu maarufu na mashuhuri mno na kwa miaka kadhaa Attar Neyshabouri alikuwa akipata elimu na maarifa kutoka kwa sheikh Aref Rukniddin Akaf. Attaf Neyshabouri aliweza kutumia nusu ya umri wake kwa kufanya safari katika miji mbalimbali, na katika safari zake hizo alifanikiwa kukutana na masheikh wakubwa wakubwa katika zama hizo, na safari hizo ziliweza kumfikisha hadi kwa sheikh Majiduddin Baghdadi. Inasemekana kuwa Sheikh Aref alipofikia marika ya uzee, Bahauddin Muhammad baba wa Jalaluddin Balkhi alikuwa pamoja na mwanawe walifanya safari ya kuelekea Iraq , wakiwa njiani walipitia Neyshabouri na wakafanikiwa kumtembelea Attar Neyshabouri, hivyo Sheikh Attar Neyshabouri alitoa nakala moja kati ya makala zake za mashairi na kumpa Jalaluddin ambapo wakati huo alikuwa bado kijana mdogo mno. --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message…
Jumatatu ya Tarehe 21 Machi 2022 Miladia inayosadifiana na tarehe (Mosi / Farvardin 1401) ni siku ya kuanza mwaka mpya wa Kiirani wa Hijria Shamsia. Siku hii ambayo hujulikana kama Nowruz , ni mwanzo wa sherehe za kale na za muda mrefu na matawi yake yameenea katika kona mbalimbali za Dunia hadi Afrika Mashariki. Asili ya sherehe za Mwaka Kogwa huko Makunduchi visiwani Zanzibar, ni sherehe hizo za Nowruzi za nchini Iran. --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message…
Jamaluddin Abu Mohammad hakuweza kupata upendo wa wazazi wake kwa muda mrefu; kwani wazazi wake walifariki dunia akiwa bado mtoto na kupata malezi akiwa mtoto yatima. Ushahidi wa kihistoria unaonyesha kuwa, Nezami Ganjavi hakuwahi kuondoka katika mji wa Ganja akiwa bado na umri mdogo, na alipofikia marika ya ujana , aliweza kujifunza sanaa na ujuzi mbalimbali na hatimaye alikuwa na ufasaha wa kuzungumza na kuandika lugha za Kiazeri, Kiarabu, Kiajemi na Kipahlavi. Nezami ni bingwa na mshairi anayepaswa kuzingatiwa kwenye mihimili na nguzo za ushairi wa Kiajemi. Yeye ni mmoja wa malenga aliyekuwa na kipaji cha kuandika mashairi na kuyasoma kwa sauti nzuri, iliyowavutia wasikilizaji. Ingawa hekaya na simulizi za hadithi za Kiajemi hazikuanzishwa na Nezami, lakini gwiji huyo anahesabiwa kuwa ni mshairi pekee aliyeweza kuendeleza ushairi wa mafumbo kwa kiwango cha juu zaidi kufikia mwisho wa karne ya sita. Nezami aliweza kujiwekea nafasi maalumu katika fasihi ya lugha ya Kifarsi inayotumika Iran na ametumia takriban miaka thelathini ya maisha yake akitunga mkusanyiko wake wa mashairi yanayoitwa "Hazina Tano" au "Khamseh". Mkusanyiko huu una mashairi matano marefu, ambayo ni: "Makhzan al-Asrar", "Khosrow na Shirin", "Lalya na Majnoon", "Haft Peykar" na "Iskander Nameh" ni hazina tano. Pia, mkusanyo wa mashairi yaliyosalia kutoka kwa Nezami ni pamoja na mashairi, mashairi ya sauti vipande ambavyo vina nafasi maalumu katika fasihi ya Kiajemi. Ingawa umaarufu mwingi wa Nezami unatokana na kutunga mashairi ya mapenzi, yenye hekima na sahili. Kwa maneno mengine, mashairi yake ni rahisi lakini ya kina, na mashairi yake yalikuwa yanamfanya mtu kufikiria na kutafakari kwa kina ili kupata siri iliyofichwa katika maneno yake. Kuna jumbe nyingi za kifalsafa ambazo zimeelezwa kwa kutumia maneno mepesi na fasaha, badala ya kutumia maneno magumu na mazito. Nyingi za beti zake za mashairi zilikuwa zikielezea maisha ya akhera, sanjari na kuyafurahia maisha mafupi ya ulimwenguni. Kuna tofauti za maoni kuhusu kuzaliwa kwa baba wa mshairi Nezami Ganjavi, na baadhi ya vyanzo vinaeleza kuwa anatoka Tafresh au Farahan. Lakini Behrouz Thorotian (mtafiti wa fasihi, mwanasayansi na profesa mstaafu) anaeleza kuwa, mwanzo wa beti za mashairi ya Layla na Majnoon, zinaonyesha kuwa alikuwa na asili ya Kiajemi. Ameendelea kusema kuwa, ubeti wa 36 wa shairi la Leyla na Majnoon, unafichua kazi na nafasi ya mshairi ambaye alikuwa Dehqan yaani “mkulima” na kuitambulisha jamii yake kuwa ni Muajemi. Kwa Wairani neno Dehqan "mkulima" linamaanisha mmiliki wa ardhi ya kilimo; malenga Ferdowsi naye katika beti zake amefafanua kuwa, tafsiri ya neno hilo lilitumika baadaye kwa Wairani wote. Kwa kuongezea, neno Dehqan "mkulima" lilitumiwa pia kwa maana ya "mwanahistoria". Kwa hivyo, inaweza kueleweka kuwa Nezami Ganjavi anajitambulisha kama malenga, mkulima wa Iran, mwanahistoria, muimbaji wa mashairi na mmiliki wa ardhi ya kilimo. Wakulima wamekuwa na jukumu la kuhifadhi tamaduni na historia ya Iran katika kipindi cha Kiislamu, na kwa ufupi, familia ya Nezami Ganjavi inaweza kuchukuliwa kuwa familia ya wakulima wenye ufahamu wa kitamaduni na utajiri wa mali ambao wamekuwa na nafasi muhimu katika fasihi. Nezami Ganjavi alikuwa mshairi mashuhuri, mwandishi wa riwaya, mwenye hekima na ambaye amekuwa na ushawishi mkubwa katika fasihi ya Kiajemi na daima ametajwa kuwa mtu muhimu katika historia. Dola la Uajemi ni moja kati ya madola makubwa yaliyokuwa yakitawala duniani. Jamhuri ya Azerbaijan, iliyoko katika eneo la Caucasia kati ya Ulaya na Asia ilikuwa chini ya himaya ya dola la Uajemi katika zama hizo. --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message…
I
Iran-Tanzania Podcast

kumbukizi ya miaka 2 ya shujaa mpigania haki na amani Haj Qassem Suleimani, ambapo aliuiliwa Shahidi na Majeshi dhalimu ya Marekeni mjiini Baghdad nchini Iraq. Kamanda Soleimani ambaye amepewa lakabu ya bwana wa mashahidi wa muqawama, katika umri wake wote uliojaa baraka na akiwa kamanda wa IRGC, alikuwa mstari wa mbele kuyasaidia na kuyaunga mkono mataifa yote yanayodhulumiwa ya Waislamu, bila ya kujali ni mataifa ya watu gani. Muhimu kwake muda wote ilikuwa ni kupigania Uislamu na mafundisho sahihi ya Qur'ani Tukufu. Shujaa huyu (Qassem Soleimani) alizaliwa tarehe 11 Machi 1957, katika kijiji cha Qanat-e Malek, Mkoa wa Kerman nchini Iran. Baada ya kumaliza masomo akiwa na umri wa miaka 18, alihamia mjini Kerman na huko aliajiriwa na Shirika la Maji la mji huo. Wakati wa harakati za mapinduzi ya Kiislamu zikiwa zimepamba moto, Qassem Soleimani alifahamiana na mwanachuoni mmoja wa kidini aliyeitwa Sheikh Reza Kamyab aliyetoka mji wa Mashhad, ulioko kaskazini mashariki mwa Iran na kwenda mjini Kerman kulingania dini, sanjari na kuelezea dhulma na ukandamizaji unaofanywa na utawala wa kifalme dhidi ya wananchi wa matabaka mbalimbali nchini humo. Kuhusiana na mauaji hayo, Ripota Maalumu wa Haki za Binadamu wa Umoja wa Mataifa (UN), Agnès Callamard amesema kuwa, mauaji ya Luteni Jenerali Qassem Soleimani ni ugaidi wa kiserikali wa Marekani na yalikiuka sheria za kimataifa na hati ya Umoja wa Mataifa. Msimamo huo wa Umoja wa Mataifa umewakasirisha sana maafisa wa serikali ya Marekani ambao waliharakisha kutetea kitendo cha mauaji hayo. Callamard ameongeza kuwa, Marekani imeshindwa kutoa ushahidi wa kutosha wa kuyapa nguvu madai yake kwamba kamanda Soleimani alikuwa tishio kwa taifa hilo. Nchi kadhaa za Kiislamu na zisizokuwa za Kiislamu, Umoja wa Mataifa na jumuiya mbalimbali za kutetea haki za binadamu duniani zililaani kitendo hicho cha kigaidi cha Marekani dhidi ya afisa wa ngazi za juu wa jeshi la Iran. Hakika sisi ni wa Mwenyezi Mungu na kwake tutarejea --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message…
I
Iran-Tanzania Podcast

MIAKA MIWILI YA KUMBUKIZI YA KIFO CHA LUTENI JENERALI QASSEM SOLEIMANI Usiku wa manane wa kuamkia Ijumaa 3 Januari Mwaka 2020, wakati anga ya jiji la Baghdad mji mkuu wa Iraq ikiwa tulivu, ghafla watu wa mji huo walishtushwa na kuamshwa na milio ya milipuko na kuwafanya waingiwe na taharuki wakidhani kuwa kundi la kigaidi la ISIS limeushambulia tena mji huo. Baada ya masaa machache, zilianza kusambaa taarifa za kuuawa Luteni Jenerali Qassem Soleimani, Kamanda wa Kikosi cha Quds cha Jeshi la Walinzi wa Mapinduzi ya Kiislamu nchini Iran IRGC, ambaye alienda nchini Iraq kwa mwaliko rasmi wa viongozi wa nchi hiyo, akiwa pamoja na Naibu Mkuu wa Harakati ya Al-Hashdu al-Sha’abi Abu Mahdi Al-Muhandis na wengine wanane waliuliwa shahidi baada ya msafara wa magari yaliyowabeba kulengwa na kushambuliwa na makombora ya majeshi ya Marekani karibu na uwanja wa ndege wa Baghdad, mji mkuu wa nchi hiyo. Kamanda Soleimani ambaye amepewa lakabu ya bwana wa mashahidi wa muqawama, katika umri wake wote uliojaa baraka na akiwa kamanda wa IRGC, alikuwa mstari wa mbele kuyasaidia na kuyaunga mkono mataifa yote yanayodhulumiwa ya Waislamu, bila ya kujali ni mataifa ya watu gani. Muhimu kwake muda wote ilikuwa ni kupigania Uislamu na mafundisho sahihi ya Qur'ani Tukufu. Shujaa huyu (Qassem Soleimani) alizaliwa tarehe 11 Machi 1957, katika kijiji cha Qanat-e Malek, Mkoa wa Kerman nchini Iran. Wakati wa harakati za mapinduzi ya Kiislamu zikiwa zimepamba moto, Qassem Soleimani alifahamiana na mwanachuoni mmoja wa kidini aliyeitwa Sheikh Reza Kamyab aliyetoka mji wa Mashhad, ulioko kaskazini mashariki mwa Iran na kwenda mjini Kerman kulingania dini, sanjari na kuelezea dhulma na ukandamizaji unaofanywa na utawala wa kifalme dhidi ya wananchi wa matabaka mbalimbali nchini humo. Qassim Soleimani alivutiwa mno na hotuba za mwanachuoni huyo zenye kuhamasisha wananchi kujitolea na kupambana na utawala wa kitaghuti uliokuwa ukitawala nchini humo. Baada ya ushindi wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (1979), Soleimani alijiunga na Kikosi cha Kulinda Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran (IRGC). Mnamo mwaka 1998, Kamanda Soleimani aliteuliwa na Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu ya Iran na ambaye pia ni Amiri Jeshi Mkuu wa majeshi yote nchini, kuwa kamanda wa Brigedi ya Quds. Katika jukumu hilo, kamanda Soleimani aliweza kuimarisha satua na ushawishi wa Iran katika eneo la magharibi mwa Asia, na hasa katika suala la kuleta mwamko wa Kiislamu na kuimarisha zaidi harakati ya Hizbullah nchini Lebanon na makundi mengine ya muqawama huko Palestina. Akiwa Mkuu wa Kikosi cha Quds, Luteni Jenerali Qassem Soleimani alifanikiwa kuliangamiza genge la kigaidi na ukufurishaji la Daesh (ISIS) katika nchi mbili za Kiarabu za Iraq na Syria na pia alifanikiwa kuwapa zawadi ya amani, utulivu na usalama wananchi wa nchi hizo mbili, kwa kuasisi kwake harakati za kujitolea za wananchi. Qassem Suleimani alipewa majukumu mbalimbali ndani na nje ya nchi, yakiwemo ya kupatanisha migogoro ya wenyewe kwa wenyewe katika nchi rafiki, na ukiwemo mgogoro ulioibuka kati ya jeshi la Iraq na kikosi cha wanamgambo wa Mahdi nchini humo, mwezi Machi 2008. Mnamo tarehe 24 Januari 2011, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu Sayyed Ali Khamenei na Amiri Jeshi Mkuu, alimpandisha cheo kamanda Qassem Soleimani, na kuwa Meja Jenerali. Ayatullah Khamenei alikuwa na uhusiano wa karibu mno na kamanda Soleimani na kufikia hatua ya kumuita "shahidi aliye hai". Mnamo Machi 2019, Kiongozi Muadhamu wa Mapinduzi ya Kiislamu alimtunuku kamanda Qassem Soleimani nishani ya "Dhul Faqar", na kumfanya kuwa kamanda wa kwanza wa kijeshi kupokea heshima hiyo, tangu ulipopatikana ushindi wa mapinduzi ya Kiislamu ya Iran mwaka 1979. --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message…
Kwa maelfu ya miaka sasa, Wairani wamekuwa wakisherehekea usiku wa mwisho wa msimu wa mapukutiko (maarufu kama Shabe Yalda) kwa kutekeleza mila na desturi katika miji mbalimbali nchini Iran, usiku unaotajwa kuwa ni mrefu zaidi wa mwaka na wenye giza nene mno. Historia inaeleza kuwa, sherehe ya usiku wa Yalda ilianza zama za kale mno, na wala haifahamiki ni muda gani hasa ilipoanza, lakini wanaakiolojia walio wengi wanaeleza kuwa, usiku huo ulianza yapata miaka elfu saba iliyopita. Happy Shabe Yalda --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message…
I
Iran-Tanzania Podcast

ujumbe wa Ayyatullah Ali Khamenei kwa Mahujaji --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message
I
Iran-Tanzania Podcast

Ten years after the migration (Hijrah), the Islamic prophet Muhammad ordered his followers to call upon people everywhere to join him in his last pilgrimage. Islamic scholars believe more than seventy thousand people followed Muhammad on his way to Mecca, where, on the fourth day of the month of Dhu'l-Hijjah, there were more than one hundred thousand Muslims present for his entry into the city. While returning from this pilgrimage, on 18 Dhu'l-Hijjah 10 AH (March 632 CE) at an area known as Ghadir Khumm, Muhammad delivered a well-known sermon during which he called up his cousin and son-in-law Ali ibn Abi Talib and declared, "to whomsoever I am Mawla, Ali is also their Mawla".it was the official designation of Ali as Muhammad's successor. As a result, the date of the sermon is considered to be one of the foundational events of Shia Islam, with the anniversary becoming one of its most important annual celebrations as "Eid al-Ghadir". --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message…
I
Iran-Tanzania Podcast

According to Islamic sources, the event of Mubahala was a meeting between the Islamic prophet Muhammad and a Christian delegation from Najran (present-day Saudi Arabia), in the month of Dhu'l-Hijja, 10 AH (October 631, October 631–32, October 632–33), where Muhammad called for invoking a curse to reveal who was lying about their religious differences. The initial effort was to invite the Najrani Christians to Islam and acknowledgement of Muhammad as a prophet. During religious discussions of similarities and differences, the topic of the divinity of 'Īsā (Jesus) arose.The Christians refused to accept Muhammad's teachings about Christ and refused denying their beliefs. Muhammad suggested invoking a mubahala (prayer curse) regarding their refusal, and included his Ahl al-Bayt in the call to invoke a curse. The Christians returned to the place they were staying. Their leader al-Sayyid, al-'Aqib advised them saying: "If he challenges us with his people, we accept the challenge for he is not a prophet; but if he challenges us with his family in particular we don't challenge him, for he is not going to put forward his family unless he is truthful." The morning of 24th Dhul Hijjah, Muhammad emerged at the appointed time. He brought only selected members of his family, carrying Husayn in his arm with Hasan holding his hand, followed by Fatima and Ali. Tradition states the Christians were surprised when they saw Muhammad's family ("Ali, Fatima, Hasan and Husayn") accompanying Muhammad. Christians were surprised and, according to the traditions, decided not to invoke a curse on Muhammad and the others. They instead asked for peace by offering Muhammad tribute in return for protection. Islamic sources offer various explanations of the outcome. Some narratives suggest the Christians would have perished by the end of the year if they had entered into the imprecations. The event is commemorated annually on 24 Dhu al-Hijjah by Shia and is an inceptual argument for Shia Muslims in proving that Ahl al-Kisaʾ (People of the Cloak) are the Ahl al-Bayt (People of the Household [of Muhammad]) mentioned in the Quran. --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message…
I
Iran-Tanzania Podcast

Historia fu ya Maisha ya Imam Khomeini R.A --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message
Jina lake ni Imam Ghiyathu-ud-Din Abu al-Fat’h Umar ibn Ibrahim Khayyam Neyshabouri alikuwa ni mmoja wa wasomi wakubwa, wa hisabati na mashairi wa Uajemi ambayo ni nchi ya Iran kwa sasa. alizaliwa huko Neishabour mwishoni mwa karne ya tano na mwanzoni mwa karne ya sita. Mwaka halisi wa kuzaliwa kwake haujulikani.. Aliitwa Khayyam kwa sababu Baba yake alikuwa akifanya kazi ya kutengene Mahema. Alikuwa ni mmoja wa wanasayansi wakubwa wa wakati wake na alikuwa na akili isiyo ya kawaida na kumbukumbu nzuri sana. Katika ujana wake alipenda sana kusoma sayansi na maarifa, falsafa, Unajimu na hisabati, masomo ambayo yalilifikisha nafasi za juu na alikuwa na ujuzi wa matibabu, kiasi kwamba inasemekana ndiye alimtibu Sultan Sanjar, ambaye aliambukizwa ugonjwa ndui akiwa mtoto. Katika uandishi wake wa mashairi alikuwa akitumia Lugha mbili ambazo ni Kiajemi au Kifarsi na Kiarabu. Pia ameandika vitabu vingi na muhimu katika upande wa Sayansi. Khayyam alikuwa na wadhifa na umaarufu mkubwa sana, na watu wa wakati wake wote walikuwa wakimsifu kwa majina makubwa kama Imam, mwanafalsafa na Hujjat al-Haq. Aliishi wakati wa utawala wa Seljuks, ambaye alitawala kutoka Khorasan hadi Kerman, Rey, Azabajani, na pia alitawala Roma, Iraq, Yemen, na Uajemi. Khayyam alitumia sehemu kubwa ya maisha yake katika mji wa Neishabour nchini Iran na aliondoka Neishabour mara mbili tu muda wote wa maisha yake. Usafiri wa kwanza ulikwenda kuhiji na safari ya pili ilienda Mji wa Rey na Bukhara. Khayyam alikuwa na ustadi sana katika unajimu, hivi kwamba kikundi cha wana astronolojia (unajimu) wa kisasa walifanya kazi naye kujenga uchunguzi wa sultan wa Seljuk, na kwa ombi la sultan wa Seljuk, aliamua kurekebisha kalenda hiyo, inayojulikana kama kalenda tukufu. Khayyam alikuwa maarufu kisayansi na kifalsafa wakati wa uhai wake na aliheshimiwa na wasomi na wanafalsafa wa wakati wake. Katika uwanja wa fasihi na mashairi, Khayyam amepata umaarufu mkubwa katika vina kwa sababu vina vyake ni rahisi na viko katika mpangilio mzuri sana, mbali na kuwa aina ya lugha ya kishairi. Wakati zinajumuisha ufasaha na usemi, vina hivyo huwa na maana nzuri na thabiti. Katika hivi vina, Khayyam alikuwa anapenda kuelezea mawazo yake ya kifalsafa kwa njia nzuri zaidi na mara nyingi alitunga vina hivi kwa kufuata mawazo yake ya falsafa na ndio sababu Khayyam alikuwa maarufu kama mshairi wa zama au enzi zake na alijulikana zaidi kama mjuzi na mwanafalsafa. Jina lake likawa mmoja wa washairi ambao walisifika ulimwenguni. Tabia nyingine ambayo imeoneshwa katika mashairi ya Khayyam ni kwamba hotuba yake imejaa unyofu na uzani. Hii ni historia kwa Ufupi kuhusu Mshairi huyu wa uajemi (Iran) Maarufu kama Khayam au Imam Ghiyathu-ud-Din Abu al-Fat’h Umar ibn Ibrahim Khayyam Asanteni kwa kusikiliza --- Send in a voice message: https://podcasters.spotify.com/pod/show/irantanzania/message…
ขอต้อนรับสู่ Player FM!
Player FM กำลังหาเว็บ